PATA KUJUA MAPISHI

NAMNA YA KUTENGENEZA CHAPATI (SINGLE BOYS & GIRLS)

NAMNA YA KUTENGENEZA CHAPATI


Unga kilo moja weka sukari kijiko kimoja cha chai pamoja na chumvi kijiko kimoja cha chai



weka mafuta ya kupikia yamoto kikombe kimoja cha chai kidogo kisha changanya



Kisha weka maji ya uvugu vugu kikombe kimoja cha chai kidogo na endelea kuchanganya








Kanda mpaka upate mchanganyiko mzuri laini na mkavu


Kata saizi ya unga ambao ukisukuma itatosha kwenye kikaango chako


huu ni muonekano wa chapati ndogo itakayoweza kuenea katika kikaango kidogo hata kwa matumizi ya nyumbani iweke kwenye kikaango cha moto  bila mafuta pika pande zote mbili


kisha weka mafuta naigeuze geuze



hii ni chapati yako imekamilika na ni laini na ina lea kama daftari na ni tamu kupita maelezo


TOA MAONI YAKO KAMA UNATAKA KUENDELEA POKEA MAFUNZO KWA NJIA YA 
MY BLOG 
Mail:arushaclan@gmail.com or Sms: +255 (0) 658859177