PATA KUJUA MAPISHI

TAMBUA UMUHIMU NA FAIDA YA KULA MATUNDA NA MBOGA MAJANI

WEWE KAMA MPISHI TAMBUA MAJUKUMU NA THAMANI YAKO YA KUA JIKONI.

TAMBUA UMUHIMU NA FAIDA YA KULA MATUNDA NA MBOGA MAJANI

WEWE KAMA MPISHI TAMBUA MAJUKUMU NA THAMANI YAKO YA KUA JIKONI.

TAMBUA UMUHIMU NA FAIDA YA KULA MATUNDA NA MBOGA MAJANI

WEWE KAMA MPISHI TAMBUA MAJUKUMU NA THAMANI YAKO YA KUA JIKONI.

TAMBUA UMUHIMU NA FAIDA YA KULA MATUNDA NA MBOGA MAJANI

WEWE KAMA MPISHI TAMBUA MAJUKUMU NA THAMANI YAKO YA KUA JIKONI.

TAMBUA UMUHIMU NA FAIDA YA KULA MATUNDA NA MBOGA MAJANI

WEWE KAMA MPISHI TAMBUA MAJUKUMU NA THAMANI YAKO YA KUA JIKONI.

MAANDAZI YA HILIKI NA TUI LA NAZI

MAANDAZI YA HILIKI NA TUI LA NAZI

MAANDAZI HAYA YANALADHA SAFI SANA KWA MLAJI NI RUKSA KUONGEZA KIUNGO AU KUPUNGUZA NA ANDAZI LAKO LITABAKI NA UBORA ULE ULE MAANA SIO WATU WOTE WANAPENDA VIUNGO.
MAHITAJI

1 kikombe cha chai kikubwa
2 Amira ya chenga kijiko kidogo cha chai
1 kilo unga wa ngano
1 hiriki kijiko kikubwa cha chakula
1 kikombe cha chai tui zito la nazi na vijiko viwili vya mafuta ya kupikia ya baridi (1 kikombe cha chai mafuta ya moto kamahutumii tui la nazi )
1 chumvi kijiko kidogo cha chai
1 maji ya moto wa wastani kikombe kikubwa cha chai


Hii ni hiriki , sukari na Amira ya chenga

Weka sukari, Amira, chumvi na hiriki katika bakuli kisha weka mafuta yakupikia vijiko viwili

kisha weka tui la nazi

Kisha changanya unga wa ngano kilo moja katika bakuli

kisha weka maji ya moto katika unga

Anza kukanda unga

Kisha sukuma unga mpaka upate unene wa saizi ya andazi unalotaka 

Kisha kata andazi kwa saizi ya andazi la ukubwa unaotaka

Haya ndio maandazi mabichi baada ya kukatwa tayari kwa kuchomwa acha yaumuke kwa dakika 10 ili utakapochoma yasijae mafuta ndani

Weka mafuta ya kupikia katika kikaango kisha yapate moto wa wastani yasiwe yamoto sana maandazi yakaungua pia hayataiva ndani


HUU NDIO MUONEKANO SAFI WA MAANDAZI YA HIRIKI NA TUI LA NAZI ENJOY NA FAMILIA YAKO KWA CHAI YA JIONI AU CHAI YA ASUBUHI KWA KITAFUNWA SAFI NA SALAMA MAANA HAKINA MAFUTA MENGI PIA CHUMVI INAAIDIA KUKIMBIZA MAFUTA KATIKA UNGA.

JINSI YA KUPIKA WALI WA BIRYAN YA KUKU, NG.OMBE AU MBUZI

JINSI YA KUPIKA WALI WA BIRYAN YA KUKU, NG.OMBE AU MBUZI

Mahitaji
1 kilo mchele wa basmati mrefu

1 kilo nyama iwe ya kuku au ng'ombe au mbuzi kata katika umbo dogo la kutosha kula kisha ichemshe na tangawizi na kitunguu swaumu, unga wa binzari (turmeric powder) pili pili manga na chumvi ili kuweka ladha nzuri. Ikisha iva itoe iweke pembeni na mchuzi wake uweke pembeni utautumia baadae.

1 kilo ya vitunguu kata slice ( mviringo)

1 kilo nyanya nyekudu zilizoiva, osha vizuri kisha katakata saizi ndogo ndogo sana

240 gram ya mafuta ya kupikia

240 gram ya samli au mafuta yeyote ya kupikia

2 maggi chicken soup cubes

3 kijiko kidogo cha chai unga wa pilipili mwekundu

1/2 kijiko kidogo cha chai unga wa binzari (turmeric powder)

3 kijiko kidogo cha chai unga wa girigilani (coriander powder)

2 kijiko kikubwa cha chakula mchanganyiko wa tangawizi na kitunguu swaumu vilivyosagwa (ginger-garlic paste )

50 gram korosho iliyo kaangwa usizisage zibaki nzima

50 gram majani ya girigilani (fresh coriander leaves, washed and chopped)

8-12 mbegu za nzima ya hiriki (green cardamoms)

4 bay leaves ( sifahamu kiswahili chake)

15 mbegu nzima ya pili pili manga (whole black peppercorns)

30 gram majani mabichi ya minti ( mint leaves )

salt kulingana na ladha yako binafsi

Jinsi ya kuanda

Weka mafuta katika sufuria yako iliyo juu ya moto tayari, kisha kaanga nyama yako iliyokwisha chemshwa mpaka iwe na rangi ya kahawia (golden brown)

Kisha itoe nyama hiyo na ichuje mafuta ili mafuta yanayobaki weka kitunguu na endelea kukaanga kwa dakika 7-10 kisha weka unga wa binzali, unga wa pili pili mwekundu, unga wa girigilani, bay leaves, mbegu za hiriki na nusu ya mbegu za pili pili manga.

Changanya vizuri mpaka utapata mchanganyiko mzuri mkavu miminia humo maji uliyotunza baada ya kuchemshia ile nyama yako na kuiweka pembeni ipoe. kisha weka nyanya fresh ndani ya sufuria yako pika mpaka maji yakauke na mafuta yaanze kuoneka kwa juu ndani ya sufuria.

Kisha weka nyama yako ndani ya sufuria pole pole halafu punguza moto acha ijipike kwa muda mpaka mchuzi wako na nyama vikamate ladha pia usisahau kuweka chumvi kulingana na ladha unayopenda.

Chukua sufuria nyingine weka mafuta ya samli na vitunguu ilivyoslice kisha kaanga na majani ya girigilani, majani ya mint na korosho funika kwa dakika 10 picha inaonyesha hapo chini, kisha weka wali wako mkavu uliokwisha oshwa vizuri na uchanganye vizuri ongeza vikombe 5 vya maji na chumvi kidogo mchele ukishaanza kuchemka funika sufuria lako na punguza moto maji yakisha kauka kiasi weka mchanganyiko wa ile nyama yako nusu tu juu ya wali wa basmati acha wali uive kabisa kisha itakua tayari kula na pakua chakula chako kikiwa cha moto




Wali wa pishori ( Basmati rice) uliokwisha iva


Wali wa pishori ( Basmati rice) uliokwisha iva ukakaangwa na vitungu na korosho


muonekano wa majani ya girigirani wakati wa kukaangwa


Nyama ya kuku iliokaangwa vizuri na viungo na nyanya ukapata mchanganyiko mzuri mzito





Muonekano halisi wa biriyani yako baada ya kuiva ikiwa imechanganyikana na nyama pia kumbuka kunamchuzi mzito na nyma ilibaki pembeni mlaji ataweza kujongezea kiasi apendacho.

Furahia chakula hiki pamoja na familia yako

TOA MAONI YAKO KAMA UNATAKA KUENDELEA POKEA MAFUNZO KWA NJIA YA 
MY BLOG 
Mail:arushaclan@gmail.com or Sms: 0658859177

NAMNA YA KUTENGENEZA KITAFUNWA CHA MAANDAZI

NAMNA YA KUTENGENEZA MAANDAZI


Chukua Amira ya chenga gram 11



Chumvi nusu kijiko kidogo cha chai


Sukari gram 250


Unga wa ngano kilo moja

Maji ya uvugu vugu nusu lita



Mafuta ya kupikia lita 2 na nusu

Weka pakiti ndogo ya amira yenye ujazo wa gramu 11 yoote kwenye unga wako wa kilo moja



Kisha weka chumvi nusu kijiko kidogo cha chai chumvi hii husaidia kupunguza mafuta ndai yaa andazi baada ya kuiva andazi lako litakua halina mafuta safi na salama kwa mlaji

Weka sukari gram 250 katika unga wako


Baada ya hapo weka mafuta ya moto ujazo wa kikombe kidogo cha chai au gr 250
 changanya vizuri mafuta bado yakiwa yamoto



Kisha weka maji ya uvuguvugu ili kuuwa ngano nakufanya amira kuweza kumuka haraka



Kanda mchanganyiko wako safi kwa kutumia nguvu na umakini mpaka mchanganyiko wako uwe laini


Mchangyanyiko wako kama uko bado ni teketeke na ulizidisha maji kidogo weka unga kiasi kisha endelea kukanda mpakja uwe mkavu na laini

Hapa safi sasa


 Shepu vizuri tayari kwa maandalizi ya kusukuma na kukata




Sukuma unga wako mpaka saizi ya unmene halisi wa andazi lako utakavyopenda liwe

Kisha tumia kitu chechote kile kukatia kwa umbo lolote lile utakalo lipenda



Yaache kwa muda wa dakika 10 baada ya kuyakata yaumuke kisha itakua tayari kwa kuyachoma


Baada ya kukata maumbo mazuri ya duara unga unaobakia unaweza viringisha maumbo tofauti kama uonavyo katika picha pia unaweza tengeneza hata herufi

 Pasaha mafuta yako katika moto wa wastani yasiwe na moto mkali utapelekea maandazi yako kuungua kisha yaweke katika moto na geuza kila mara ili yasivimbe upande mmoja na ikawa vigumu kuyageuza




Hili ni anfazi lako safi limeshaiva na halina mafuta ndani na safi kabisa

TOA MAONI YAKO KAMA UNATAKA KUENDELEA POKEA MAFUNZO KWA NJIA YA 
MY BLOG 
Mail:arushaclan@gmail.com or Sms: 0658859177

UTENGENEZAJI WA ICE CREAM BILA YA KUTUMIA MASHINE

UTENGENEZAJI WA ICE CREAM BILA YA KUTUMIA MASHINE

Ice cream ni kifunga hamu ya kula ( Dessert ) moja wapo nzuri sana na inaweza kuliwa na watu wa lika zote pia unaweza kula ice cream muda wowote ule utakaojisikia na ukafurahia hasa ukiangalia hali ya joto inayopatikana nchini kwetu. Fata maelezo hapochini jinsi ya kutengeneza pamoja na mahitaji ili ufanikishe uandaaji wako.

Vitu vya kuandaa.

Maziwa ml 240
Sukari ml 240
Chumvi kijiko kidogo cha chai robo (1/4)
Vanilla ya maji kijiko kikubwa cha chakula 1/2
Vanilla ya mti ml 120
Low fat maziwa ml 120
low fat cream ml 120
Whipping cream yenye ubaridi wa wastan ml 480
Biskuti zilizochovywa Chocolate cream ml 480


Badala ya biskuti zilizochovywa na chocolate cream unaweza weka vipande vya chocolate, unaweza weka mchanganyiko wa ladha mabalimabli mfano matunda kama strawbery, cherry, Embe kwa kuchanganya kiasi cha ml 480 kama inavyoonyehs hapo juu katika mtiririko wa vitu vya kuandaa.



Vunja vunja vipande vya biscuti vilivyochovywa na chocolate weka pembeni safi ukisubiri baadae kidogo kuzitumia.



Weka maziwa katika sufuria nzito kwenye jiko lenye moto wa wastan acha yachemke pole pole mpaka yatakapotoa mapovu pemebi ya sufuria yatoe na weka pembeni yapoe.


Baada ya kutoa maziwa katika moto na kuyaweka pembeni yapoe changanya sukari na chumvi ndani yake


Koroga vizuri maziwa hayo mpaka sukari na chumvi viyeyuke vizuri



Changanya tena whiping cream na vanillah kwenye maziwa yale pole pole kisha changanya maziwa na ile cream vilivybaki ambavyo vyote vinamafuta kiasi ( low fat ) mpaka ichanganyike vizuri.



Kisha mimina mchanganyiko wako wote kwenye bakuli safi la kioo ili uweze kupoa na kuganda

Baada ya kumimina katika bakuli chukua bakuli jingine kubwa kiasi ya lile lenye mchanganyiko wako kwajili ya kugandisha kua ice cream. Weka barafu katika bakuli hilo kisha weka juu yake bakuli lenye mchanganyiko wako. Baada ya mchanganyiko wako kupoa kabisa chukua plastic wrap funika bakuli lako vizuri na weka katika friji kwa masaa 4 au hata masaa 24 kwa kuweka mchanganyijo wako ndani ya friji itasaidia sana kubadilisha mchanganyiko kua rojo rojo au mzito na inakua rahisi kukoroga tena ili upate umbile halisi la ice cream na laini kwa mlaji.




Baada ya masaa 4 au masaa 24 toa mchanganyiko wako kwenye friji kisha koroga vizuri na mwikosafi wa mbao au kijiko kikubwa.


Kisha funika tena na plastic wrap au foil kitu chochote kitakachozui hewa kuingia katika bakuli lako tayari kwa kugandisha kwenye freezer. Baada ya hapo weka bakuli lako katika freezer na ruhusu mchanganyiko wako ukae kwa masaa 2 kwenye freezer kisha utoe.



Baada ya kutoa mchanganyiko wako katika freezer tumia mashine ya kuchapia au unaweza tumia mchapo wa chuma au unaweza tumia uma ya kulia chakula na kukoroga vizuri mchanganyiko amabao utakua tayari umeshaanza kuganda lengo ni kuvunjavunja mapande ambayo yameshaanza kuganda. Kisha funika na plastic wraptena na rudisha katika freezer kwa masaa 2.



Baada ya masaa 2 toa mchanganyiko wako na koroga kwa kutumia mashine au uma yakulia chakula. Ice cream yako itakua nzito safi lakini bado kwa kuweza kuchota na kuliwa, kama mchanganyiko bado haujaganda vizuri kutokana na nguvu ya freezer rudisha kwenye freezer igande tena kwa muda kiasi.



Baada ya ice cream yako kua imeganda vizuri chukua zile bisckuti zenye chocolate tupia katika mchanganyiko wako wa ice cream na uchanganye vizuri sana kwa umakini, aidha inaweza kua ni matunda ya ladha yeyote badala ya biskuti bado itapendeza na utakua umebadilisha ladha.


Kisha chukua chombo cha plastic kisafi na kikavu, weka mchanganyiko wako ndani yake na hakikisha unaacha nafasi ya inchi 1 au 1/2 inchi kwajili ya kutanuka.



Kisha funika vizuri plastic yako na mfuniko safi na uirudishe katika freezer iweze kuganda kabisa mpaka itakapokua ngumu.



Baada ya ice cream kua ngumu toa kwenye freezer fungua chombo chako cha plastik na tumia chombo maalumu cha kuchotea ice cream vipo vingi sana hapa nyumbani tanzania vinauzwa kwenye supermaket. Chota maumbo mazuri sana ya mviringo kisha weka kwenye bakuli au glasi ya udongo na ufurahie ice cream yako!!


NATUMAI MPAKA HAPO MTAKUA MMEELEWA VIZURI SANA SOMO HILI LA LEO NA KUWEZA KUTENGENEZA ICE CREAM SAFI KABISA WATOTO, BABA AU MGENI AKAFURAIA SANA CHAKULA HIKI CHEPESI.

NAOMBA MTENGENEZE KWAKUFATA MAELEKEZO VIZURI HALAFU MNIPATIE MATOKEA KISHA TUENDELEE NA SOMO BAADA YA KUTENGENEZA ICE CREAM HIYO UTAIPAMBA VIPI TUTAFANYA UPAMBAJI WA AINA TOFAUTI ZENYE LADHA MBALIMBALI YA ICE CREAM AINA 10 HADI 20.


TOA MAONI YAKO KAMA UNATAKA KUENDELEA POKEA MAFUNZO KWA NJIA YA 
MY BLOG 
Mail:arushaclan@gmail.com or Sms: 0658859177